Sunday, 16 June 2013

Ujerumani yampiga jeki mkaguzi mkuu wa Serikali

Kwa ufupi
Akizungumza jana wakati wa kusaini makubaliano ya msaada huo ambao umetolewa kupitia Shirika la Misaada la Ujerumani (GIZ), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, alisema msaada huo wa Euro 3.5 milioni utakwenda katika maeneo mbalimbali ya ukaguzi na kwamba mradi huo utakuwa wa miaka minne.
Dar es Salaam. Serikali ya Ujerumani imetoa msaada wa zaidi ya Sh7 bilioni kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za ukaguzi zinazofanywa na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT).
Akizungumza jana wakati wa kusaini makubaliano ya msaada huo ambao umetolewa kupitia Shirika la Misaada la Ujerumani (GIZ), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, alisema msaada huo wa Euro 3.5 milioni utakwenda katika maeneo mbalimbali ya ukaguzi na kwamba mradi huo utakuwa wa miaka minne.
Alisema lengo la msaada huo ni kuboresha utendaji wa ofisi hiyo na kuhakikisha inatimiza wajibu wake kwa ufanisi katika ngazi ya kitaifa na kimataifa pamoja na kuboresha uhusiano na wadau wakuu wa nje. Alisema pia fedha hizo zitasaidia kuikagua Serikali na misaada wanayopewa na wafadhili ikiwamo Ujerumani.
“Msaada huu umekuja wakati muafaka hasa ikizingatiwa kuwa tangu Julai mwaka jana tumeanza shughuli za ukagu

No comments:

Post a Comment