Sunday, 16 June 2013

Morocco yashinda,kundi lazidi kuwa gumu.

Timu ya Taifa ya Morocco jana ilifanikiwa kuifunga timu ya Taifa ya Gambia kwa magoli 2-0 na kuipiku Tanzania katika msimamo wa Kundi C.
Mpambano ulikuwa mkali na Morocco walifanikiwa  kupata goli la kwanza katika dakika ya 3 kupitia kwa Barrada na kipindi cha pili Belhanda akaipatia goli la pili ikiwa ni dakika ya 51 ya mchezo,na kuiacha kabisa Gambia kuendelea kushika mkia kwa kuwa na pointi moja.
Kwa matokeo hayo Morocco sasa wanapanda hadi nafasi ya pili wakiwa na pointi 8 wakiachwa kwa pointi mbili na vinara wa kundi hilo Ivory Coast wenye pointi 10 ambao leo watakuwa wageni wa Timu ya Taifa ya Tanzania watakapopambana pale Jijini Dar es Salaam.
Pia matokeo hayo yanaifanya timu ya Taifa ya Tanzania maarufu kwa Taifa Stars kurudi hadi nafasi ya tatu ikiwa na pointi 6 ivo itahitaji kucheza kwa kujituma zaidi ili washinde katika mchezo wa leo na kujiweka katika nafasi nzuri yakuwania kufuzu kwa  kombe la Dunia mwakani 2014 litakalofanyika nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment