Wednesday, 26 June 2013

MLIPUKO WA BOMU JIJINI ARUSHA: CHAMA CHA CHADEMA KUFUTWA KATIKA RAMANI YA SIASA.....!!


JOHN TENDWA




Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania Mh. 'John Tendwa' ametaja kukifuta chama cha siasa cha CHADEMA endapo kitabainika kuwa ndio waliohusika katika kulipua bomu katika mkutano wao wa 15/06/2013 huko jijini Arusha na kusababisha vifo na majeruhi kadhaa. Tendwa  ameyasema   hayo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Hot Mix cha EATV akijibu swali la mtangazaji wa kipindi Adrian Stepp  kuhusu  hatua  zitakazochukuliwa baada ya kutokea kwa tukio hilo jijini humo.





Alipoulizwa kama itathibitika kuwa CCM ndio walihusika kulipua bomu hilo amedai kuwa hawezi kukifuta kwakuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kufanya mapinduzi ya kalamu. Baada ya kauli hii ya Mh. 'Tendwa' mijadala kadhaa iliibuka kwenye mitandao hususani kwenye mtandao wa jamiiforum wakikosoa kauli hiyo.

ZINEDINE ZIDANE ATEULIWA KOCHA MSAIDIZI WA REAL MADRID - ATAMBULISHWA PAMOJA NA CARLO ANCELOTTI


Real Madrid wamemtambulisha rasmi kocha wao mpya Carlo Ancelotti na pia wametangaza kwamba Zinedine Zidane na Paul Clement watakuwa ndio makocha wasaidizi.

Ancelotti alitambulishwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu na raisi wa klabu hiyo Florentino Perez mapema leo mchana.
 
Ancelotti atasaini rasmi mkataba wa miaka mitatu na Madrid July 3 akitokea Paris St Germain.



AFANDE SELE NAE AFUNGUKA KUHUSU SAKATA LA OMMY DIMPOZ KUMTUKANA ALBERT MANGWAIR


MSANII wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi 'Afande Sele' amuombea msamaha msanii wa muziki Omary Faraja 'Ommy Dimpozi' kutokana na kauli yake aliyeitoa inayodaiwa kumkashifu marehemu Alberty Mangwea 'Ngwair'.

Msamaha huo umetokana na kauli aliyeitoa msanii Ommy Dimpozi kudai kuwa hawezi kufa maskini kama msanii Ngwair.

Afande Sele alidai kuwa kauli hiyo haikuwa mbaya ingawa watanzania hawakuilewa hivyo Ommy ametereza ulimi na anapaswa kusamehewa kama binadamu anapokosea.

Alisema kauli yake ilikuwa inamaanisha wasanii wanatakiwa wapate haki za msingi na siyo kutumiwa huku wengine wakiendelea kunufaika na wao kudidimia na hali ngumu ya kimaisha.

"Hatuwezi kuendelea kufanya hivyo mimi namuombea msamaha kwa watanzania kauli yake ilikuwa na lengo zuri ila ameshindwa kuifikisha vyema hivyo ameteleza inabidi tumsamehe ili mambo mengine yaendele" alisema Sele.

Wakati huo huo bado ile  kauli anayodaiwa kuitoa msanii huyo Ommy Dimpozi' inaendelea kumtesa na kusababisha kushindwa kuwapa burudani mashabiki zake.

Ommy  Dimpozi alipata wakati mgumu baada ya kufanyiwa fujo na mashabiki alipokuwa akifanya shoo pamoja na wasanii wenzake walioshiriki katika Tuzo za Kilimanjaro mwaka huu wakiwa mjini Dodoma.

Msanii huyo anadaiwa kutoa kauli hiyo hivi karibuni ambapo alisema hataki kufa masikini kama ilivyokuwa kwa msanii wa Hip hop Albert Magwear.

Kauli hiyo iliwachukiza baadhi ya mashabiki wa muziki waishio mjini Dodoma ambapo msanii Magwear alisoma na kukulia katika mji huo.

Msanii huyo atazidi kuwa na wasiwasi kwa baadhi ya mikoa atakayozunguka kufanya shoo zake ikiwemo mkoa wa Morogoro ambapo ndio familia ya msanii huyo inapoishi.

Alipotafuta na mwandishi wa habari hili kuzungumzia ishu hiyo Dimpozi alisema hayuko tayari kusema chochote kinachohusiana na shoo yake ya Dodoma na hataki kumzungumzia Magwear.

ASANTE KWA KUNIPA MCHANGO WAKO WA KUPITIA BLOG HII




MAJAMBAZI WAVAMIA KITUO CHA MAFUTA ORYX MAKAMBAKO WAPORA MAMILIONI YA SHILINGI WAUA WALINZI WAWILI WAJERUHI MENEJA


Focas Malengo Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe
.....................................................................................................................

Watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wakiwa na silaha mbali mbali zikiwemo wa moto wamevamia kituo cha Mafuta cha Oreyx kilichopo mjini Mkambako mkoa wa Njombe na kufanya mauwaji ya kinyama kwa walinzi wawili na kujeruhi mmoja kabla ya kupora kiasi cha zaidi ya Tsh milioni 7

Mashuhuda wa tukio hilo wameueleza mtandao huu kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana .

Mashuhuda hao walisema kuwa majambazi hao wawili wakiwa na usafiri wa piki piki ambapo walifika katika kituo hicho kwa ajili ya kununua mafuta ya Tsh 5000 na wakati wakiendelea kuhudumiwa ghafla walianza kuwashambulia walinzi kwa risasi na kuwaua walinzi wawili na kumjeruhi meneja wa kituo hicho.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Focas Malenge amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliouwawa kuwa ni Jonas Mpogole na Chesco Sanga ambao ni walinzi wa kampuni ya ulinzi ya Makambako .

Mbali ya kuwaua walinzi hao wawili pia majambazi hayo yalimjeruhi kwa risasi meneja wa kituo hicho Jonas Msenyi na kupora fedha zaidi ya Tsh milioni 7

Alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea na msako wa kuwasaka majambazi hayo ikiwa ni pamoja na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo la polisi

NIKUMBATIE 'AM READY TO FLY' FEAT. FUNDI SAMWELI IJUMAA HII NDANI YA AMBASSADORS LOUNGE

POLISI JIJINI DAR WAKAMATA WATU WAWILI WAKIWA NA BASTOLA KATIKA PIKIPIKI


Askari kanzu (kulia) akiwa ameshika bastola aliyokutwa nayo mtu mmoja aliyekuwa amepakiwa katika pikipiki aina ya Boxer yenye namba za usaji T 961 CJW katika mtaa wa Makunganya jirani kabisa na benki ya Posta jijini Dar es Salaam mchana huu. Kutokana na kuongezeka kwa matukio ya ujambazi wa kutumia pikipiki Polisi wameimarisha ulinzi na hasa katika maeneo ya mabenki.
TOA MAONI YAKO HAPA

Ulinzi wa Obama Dar

obama

Dar es Salaam. Maandalizi ya ujio wa Rais wa Marekani, Barack Obama nchini yanazidi kupamba moto huku maofisa wa usalama wa Marekani wakipiga kambi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Aidha, kutokana na ujio huo, Serikali imeagiza mashirika yote ya ndege kubadili ratiba zao za safari Julai Mosi, siku ambayo Rais huo atatua nchini.
Jana, waandishi wetu walishuhudia pilikapilika za kuimarisha ulinzi katika uwanja huo jambo ambalo uongozi wa uwanja huo jambo wamelieleza kwamba halijawahi kutokea.
Ulinzi haujawahi kutokea
Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Moses Malaki alisema jana kwamba ratiba za uwanjani hapo zitabadilika kutokana na uzito wa ugeni huo.
Alisema kwa kawaida anapokuja kiongozi mkubwa wa kitaifa katika uwanja huo hakuna ndege inayoruhusiwa kutua kwa kipindi cha nusu saa.
“Ni kweli hali hiyo pia itakuwapo atakapokuja Rais Obama na safari za ndege zitabadilika kulingana na ratiba ya kutua na kuondoka kwa Rais huyo,” alisema Malaki.
Pia alisema ulinzi katika uwanja huo umeimarishwa kwa mwezi mmoja sasa na tangu wakati huo, maofisa wa usalama wa Marekani wamekuwa wakifika kwa nyakati mbalimbali.
“Sijawahi kuona ulinzi mkali kama huu, wamekuja marais wengi hapa nchini lakini ulinzi huu ni wa kutisha, sijui kwa sababu gani?” alisema Malaki.
Alisema awali, wakati maofisa hao walipoanza kuwasili nchini hawakutambua ni mgeni gani anayetarajia kufika lakini baadaye walipelekewa taarifa kuwa ni Rais Obama na baadaye walitaarifiwa kuwa angetua saa 8.40 mchana, Julai Mosi.
Mkurugenzi huyo alisema Rais Obama atakuja na ndege nne, moja itakayombeba, ya pili kwa ajili ya mizigo, ya tatu itakuwa ya waandishi wa habari na maofisa wa usalama na ya mwisho ni kwa ajili ya dharura ambayo itaegeshwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Malaki alisema maofisa wa Marekani wanaowasili nchini wamekuwa wakifanya shughuli mbalimbali za kuhakikisha kuwa hali ya usalama inaimarishwa na kuwaacha wazawa wakifanya shughuli za kawaida.
“Ulinzi ni mkali mno, yapo masharti kadhaa wanayoyataja kuwa yatatumika kwa watu watakaoingia eneo la uwanja au kuisogelea ndege ya Rais Obama. Jamaa wameweka masharti magumu,” alisema.
Mkurugenzi huyo alisema maofisa hao wanakuja kwa makundi na hivi karibuni lilifika kundi la kusimamia mawasiliano ambayo yatatumiwa wakati watakapokuwa nchini.
“Pia wamechukua kwa muda karakana ya Shirika la Ndege la Precision Air iliyoko kwenye eneo la Uwanja wa Ndege. Maofisa wa Usalama wa Marekani wanataka kufanya shughuli ndani mle,” alisema Malaki.
Pia, ndege mbovu zilizokuwa kwenye maeneo ya uwanja huo zimeondolewa. Viongozi wa Precision Air hawakupatikana kuzungumzia suala hilo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Fadhili Manongi alisema ni utaratibu wa kawaida kwa karakana kuazimwa wakati wanapokuja wageni mashuhuri.
“Nafasi ile mara nyingi hutumiwa na maofisa wa usalama pale wanapokuja wageni mashuhuri kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere,” alisema.
Alidokeza pia pamoja na ugeni wa Rais Obama, pia kumekuwa kuna presha ya ugeni wa marais wa nchi mbalimbali duniani wanaokuja kuhudhuria mkutano wa Smart Partnership unaonza keshokutwa.
Pia wana kazi ya kuwapokea wake za marais wa Afrika watakaokutana na mke wa Rais Obama, Michelle na mke wa Rais wa zamani wa nchi hiyo, George Bush, Laura.
Kazi inayofanyika
Ofisa mmoja wa Uwanja Ndege ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema maofisa hao walifanya ukaguzi wa hali ya juu kwenye sehemu mbalimbali za uwanja huo wakitumia mitambo maalumu ya kung’amua mabomu.
“Hawa jamaa wako juu sana katika mambo ya usalama maana wana kifaa cha kuchunguza mabomu hata yaliyo chini ya ardhi,” alisema na kuongeza kuwa licha ya kukagua uwanja huo, pia walikwenda mbali zaidi na kukagua maeneo ya jirani.
Mitambo mbalimbali ya shughuli za usalama imefungwa kwenye eneo hilo la uwanja na maofisa wa Marekani walionekana wakiwa juu ya paa la moja ya majengo ya uwanja huo wakifunga mitambo katika minara mirefu kwa ajili ya kuimarisha mawasiliano.
Yavuruga ratiba za ndege
Manongi alisema kampuni za ndege zimeagizwa kufanya mabadiliko ya ratiba za safari siku atakapowasili Rais Obama ili kutoa nafasi kwa anga hilo kutumika kwa shughuli za mapokezi yake.
Alisema kampuni zote za ndege zimeshapewa taarifa kuhusu hatua hiyo.
“Kubadilishwa kwa ratiba kunatokea mara kwa mara na huwa tunawapa taarifa kampuni za ndege mapema ili wajue namna ya kujipanga,” alisema Manongi.
Kutua Senegal leo
Rais Obama anatarajiwa kuanza ziara yake ya barani Afrika leo na alitarajiwa kutua Dakar, Senegal saa 9.30 alasiri kwa saa za Afrika Mashariki.
Akiwa nchini humo, ratiba inaonyesha kuwa atakuwa na mazungumzo na Rais wa Senegal, Macky Sall kwenye Ikulu ya nchi hiyo. Pia ratiba hiyo inaonyesha kuwa atakutana na majaji kutoka mikoa yote ya nchi hiyo.
Pia atakwenda katika Kisiwa cha Goree ambacho kiko kwenye Bahari ya Atlantic na atatembelea Jumba la Makumbusho katika kisiwa hicho ambacho kilikuwa kituo cha kuhifadhi watumwa waliokuwa wanasafirishwa kutoka Afrika kwenda Marekani.
“Baada ya shughuli hiyo, Rais Obama atahudhuria dhifa ya taifa kabla ya kupumzika kwa muda mfupi na kuanza safari ya kwenda Afrika Kusini,” ilisema taarifa hiyo ya Ikulu ya Marekani.
Source:Mwananchi

SERIKALI YATOA TAMKO KUHUSU KAULI YA WAZIRI MKUU...YADAI POLISI WANARUHUSIWA KUPIGA NA KUUA KISHERIA



Serikali imetoa tamko bungeni kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi ikieleza kuwa sheria ya kanuni ya adhabu inaruhusu kutumia nguvu za kadiri hata kiasi cha kusababisha madhara au kifo.


Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kunukuliwa bungeni akiwataka polisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote wanaokaidi kutii sheria.

“…Nasema wapigwe tu, maana tumechoka sasa,” alisema Pinda alipojibu maswali ya papo hapo Alhamisi iliyopita.


Akisoma tamko hilo bungeni jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alisema kuwa kifungu cha 18(B) na 18(C) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kinatoa uwezo kisheria wa kutumia nguvu za kadiri hata ikibidi kiasi cha kusababisha madhara au kifo katika mazingira ya kisheria.


Aliyataja mazingira hayo kuwa ni pamoja na kuokoa uhai wa mtu mwingine, kuzuia madhara makubwa ya mwili yasitokee kwake au kwa mtu mwingine na kumzuia mtu anayetenda tendo ovu la kubaka au kunajisi mtoto au kufanya vitendo kinyume na maumbile.

Pia kumzuia mtu anayevunja nyumba usiku au unyang’anyi wa kutumia silaha au kuchoma nyumba moto au kufanya kitendo chochote kinachohatarisha uhai wa mtu au mali.


Alieleza kuwa Kifungu cha 18 na 18(A) cha Sheria ya Adhabu Sura namba16 iliyofanyiwa mapitio mwaka 2002, kinampa haki mtu yeyote akiwemo askari kujilinda, kumlinda mtu mwingine, kulinda mali yake au mali ya mtu mwingine ikiwemo ya Serikali na taasisi zake, ambayo iko chini ya uangalizi wake kisheria.


Kauli hiyo ya Serikali kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi, ilitolewa ikiwa ni ufafanuzi wa jibu la swali la nyongeza lililoulizwa bungeni Mei 28,2013 na Rashir Ally Abdalah (Tumbe-CUF), ambapo Silima alisema mauaji yanayofanywa na askari polisi ni mauaji ya kisheria. 


Kutokana na kauli hiyo, Mbunge wa Wawi, Hamad Rashi Mohammed aliomba mwongozo wa spika kupata ufafanuzi wa kauli hiyo, na jana Silima kutoa kauli ya Serikali kujibu mwongozo huo.

“Ikumbukwe pia kuwa, kifungu cha 29 cha Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi wasaidizi Sura322, pamoja na Kanuni za Kudumu za Utendaji za Jeshi la Polisi Na274, vinampa haki ya kisheria askari polisi kubeba na kutumia silaha za moto ikiwamo bunduki na mabomu katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku..,”alisema Silima.


Alifafanua kwamba katika kutafsiri sheria, kanuni na taratibu mbalimbali ikiwamo alizozitaja, mahakama katika nyakati tofauti imetoa msimamo wa kisheria juu ya suala hilo.


Akitoa mfano alisema: “Mathalan katika kesi ya Seif Mohamed Senzagala dhidi ya Jamhuri ya mwaka 1994 kama ilivyonukuliwa na Tanzania Law Report ukurasa wa 122, ambapo mshitakiwa (mwomba rufaa) alimjeruhi kwa panga mlalamikaji ambaye alimfuata nyumbani kwake na kuanza kumshambulia.”


Alisema katika kesi hiyo,mahakama ya rufaa pamoja na kuridhia uamuzi wa mahakama ya awali wa kumtia hatiani kwa kutumia nguvu kupita kiasi, ilibainisha kuwa mshtakiwa hakustahili adhabu kwani alitenda kosa lile wakati akijihami dhidi ya mashambulizi toka kwa mlalamikaji.

“Kwa msingi huo, tarehe 28 Mei, 2013 wakati nikijibu swali Na 290, nilitumia maneno ‘mauaji yanayofanywa kisheria’ nikimaanisha mauaji yanayotokea katika mazingira niliyoeleza..,”alisema Silima.

Hata hivyo alisema siyo nia ya Serikali kuhalalisha vitendo vya matumizi mabaya ya silaha ambavyo vinaweza kufanywa na askari wasio waadilifu.

Alibainisha kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, kuheshimu haki za raia na kutumia busara kutatua migogoro.

Hata hivyo, Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni imelaani kauli ya Serikali kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi iliyoitoa jana na kueleza kuwa haikubaliani nayo kwa kuwa inatoa baraka kwa polisi kuendeleza mauaji ya raia.

Akizungumza na mwandishi wetu baada ya kikao cha bunge kuahirishwa, Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani wa kambi hiyo rasmi, Vicent Nyerere alisema kauli hiyo ingekuwa na uthabiti kama askari polisi wangekuwa waadilifu.


“Kauli ingekuwa thabiti kama polisi wangekuwa waadilifu. kabla ya kutoa kauli hiyo, Serikali ilitakiwa kuchuja miongoni mwa askari wa jeshi la polisi, wa ngazi zote na kuwaondoa wasio waaadilifu ndipo wakatoa kauli hiyo wananchi wataielewa Serikali,”alisema Nyerere ambaye pia ni Mbunge wa Musoma Mjini(Chadema).


Kwa upande wake, Mbunge wa Ole, (CUF) Rajab Mbarouk Mohammed akizungumzia kauli hiyo ya Serikali alisema kuwa majibu ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima ni ya kisiasa.


Alisema kwamba kauli hiyo ni mwendelezo wa kauli iliyotolewa Alhamisi iliyopita na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiwataka pilisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote watakaokaidi kutii sheria.


“Hakuna mwenye haki ya kuua, kuua ni kuua tu. Mahakama pekee ndiyo ina haki ya kuhukumu kifo baada ya kumtia hatiani mshtakiwa husika. Lakini kuwa polisi wanafundishwa utii, siyo kuua,”alisema Rajab.

Alifafanua kuwa kazi ya polisi ni kulinda raia na mali zao na kwamba kuruhusiwa kujihami haimaanishi kuua raia.
Nao Wabunge Aeshi Hilaly na Aly Keissy walisema ni vizuri raia wakatii mamlaka iliyopo na kutekeleza utii wa sheria bila shuruti.

Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu alisema: “Maoni yangu haki za watuhumiwa lazima ziheshimiwe.”

Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, (TLS), Francis Stola alisema hakuna sheria inayompa mamlaka askari polisi kutumia nguvu za ziada ikiwemo kupiga raia pindi anapotekeleza majukumu yake,isipokuwa tu anaweza kutumia nguvu kiasi iwapo raia anayekabiliana naye anaonyesha vitendo vya kukaidi amri ama kuhatarisha usalama.


Stola ambaye alikuwa akitoa ufafanuzi wa kisheria kuhusiana na kauli bungeni alisema kuwa kwa kufuata sheria polisi haruhusiwi kupiga raia. “ Ukisoma sheria hakuna mahala utakuta kuna neno limeandika piga…. Askari polisi anachoweza kufanya ni arrest(kamata) na siyo vinginevyo, hana mamlaka kabisa ya kupiga raia”

Alisema sheria imetamka wazi kuwa kunapojitokeza hali yoyote inayopaswa kdhibitiwa na vikosi vya ulinzi, nguvu inayopaswa kutumika ni ile ya kawaida na kwamba kitendo cha kutumia risasi za moto ama kupiga raia ni ukiukwaji wa sheria za nchi.

Alisema polisi anapaswa kutoa mwongozo kwa raia kumwelekeza jambo la kufanya iwapo kunajitokeza hali ya sintofahamu,lakini hapaswi kutumia nguvu kupita kiasi ikiwemo kuwapiga raia

“ Sheria inasema wazi kwamba panapojitokeza hali yoyote korofi, polisi wanatakiwa kutumia nguvu ya kawaida tu kukabiliana na hali hiyo na wala siyo kutumia silaha za moto… silaha za moto zinaweza kutumika tu iwapo kunajitokeza tukio ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa maisha ama mali isipotee” alisema

Kuhusu wananchi kufanya maandamano, rais huyo alisema maandamano ni haki ya msingi ya kila raia,lakini yanafanyika katika utaratibu maalumu. “ maandamano ni haki ya kila raia lakini panapaswa kuwa na utaratibu maalumu…. Kama kunajitokeza maandamano ambayo hayana utaratibu polisi wanapaswa kutumia reasonable force (nguvu ya kawaida) kudhibiti maandamano hayo na wala siyo kutumia nguvu za ziada.
 Mwananchi:

Monday, 24 June 2013

CHIGWA COMING SOON..........!!!!!!!!!!!!!!!!1


MwanaFA..AJUTA KUANZISHA BIFU NA JIDE,,APOTEZA MASHABIKI,HANA RAHA AAMUA KUFUNGUKA..SOMA ALICHOKIANDIKA HAPA


Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.
 


Mwanamuziki Hamis Mwinjuma, maarufu Mwana FA, amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee, baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake
kuna jina la Jay Dee.

Tofauti na ilivyozooeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee ‘Anaconda’, hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.

Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kurudia wimbo huo na alipofika katika kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi huo ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.

Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka; “Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapatana,” alisema Mwana FA.

Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa kama 250 tu.

Thursday, 20 June 2013

KAWA HUJAWAI TAZAMA PICHA ZA UTUPU ZA VIDEO QUEEN WA JAMBO JAMBO YA STEVE R&B



WAKATI mabinti wengi hasa mastaa wa Bongo wakijuta baada ya picha zao za utupu walizopigwa na wapenzi wao kuvuja, kwa msanii mrembo aliyepamba video ya wimbo wa Bongo Fleva uitwao Jambojambo wa msanii Steve R&B, Aisha Firozi ‘Sapna’ ni kawaida kwani hujifotoa mwenyewe.

Chanzo makini cha Risasi kimewasilisha folda lenye picha za kutosha za mrembo huyo akiwa mtupu huku kikieleza kwamba ni mchezo wake kujipiga mwenyewe picha hizo.


Kwa sharti la kutochorwa jina lake , chanzo hicho ambacho kipo aribu na Sapna kilisema: “Yule ni mtu wangu wa karibu sana, lakini tabia yake kwa kweli huwa siipendi kabisa. Anajipiga picha chafu mwenyewe, kwake ni starehe kubwa, huwezi kuamini.”

Kikiendelea ufunguka zaidi, chanzo hicho kilipasha kuwa, picha hizo amejipiga hivi karibuni nyumbani kwa rafiki yake aitwaye Doreen, Tabata - Magengeni jijini Dar es Salaam, ambapo alikuwa akiishi naye.

KAULI YA SAPNA.....
Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni; Sapna alipopigiwa simu na kuelezwa kuhusu kunaswa kwa picha hizo, kwanza alishangaa lakini akakiri kuzitambua.

“Hizo kweli ni picha zangu na nilijipiga mwenyewe sasa sijui wewe umezipataje na zimefi kaje huko kwenu? Mimi nilipiga kwa masilahi yangu mwenyewe, huwa natamani sana kujiangalia jinsi umbo langu lilivyo, ndiyo maana niliamua kujipiga na si vinginevyo.


“Kila mtu na maisha yake na mimi sikuwa na dhamira mbaya kujipiga picha hizo zaidi ya kujiangalia tu nilivyo,” alisema Sapna.

Sunday, 16 June 2013

Shilole aalikwa kwenda kupiga shoo marekani. Kuondoka hivi karibuni

Shilole aalikwa kwenda kupiga shoo marekani. Kuondoka hivi karibuni
Mwigizaji na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya Zena Mohamedi ama Shilole amepata mwaliko wa kwenda nchini Marekani kufanya shoo za mziki hivi karibuni.
Akizungumza na mwandishi wetu tokea ukumbi wa blue pearl wakati wa tuzo za filamu nchini Shilole amesema kuwa yupo kwenye maandalizi ya mwisho kwa ajili ya shoo hiyo ambayo anatarajiwa kuifanya kwenye miji miwili nchini humo.

WANAKILINGE SASA MBEYA WAKAZI WA MBEYA KAZI KWENU KUSIKIA MITAMBAO YA WANAHARAKATI HAO

Mbeya The Green City tarehe 21st June 2013 Nikki Mbishi,One the incredible na Songa watakuwa Club The Vibe,tukutane pale!!!

MLIPUKO WAMKATA VIGANJA MWENDESHA PIKIPIKI DAR...


Mkazi wa Mbagala Chemichem, Abdul Said ambaye ni mwendesha pikipiki amekatika viganja vya mikono miwili baada ya kulipukiw a na kitu alichopewa kushika.
Hata hivyo Said anashikiliwa na polisi na mwenzake mwingine ambaye hakutajwa jina baada ya kukamatwa katika maeneo ya Mbagala jana saa 6:00 usiku.
Kamishna wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova, alisema watu hao wawili walikamatwa katika maeneo hayo huku wenzao wawili wakipata upenyo na kukimbia.
Alisema dereva huyo wa pikipiki ambaye alikabidhiwa kitu mkononi ambacho ghafla kililipuka na kumkata viganja vya mikono yote miwili.
Alisema jitihada za kuwatafuta watuhumiwa wengine wawili bado zinaendelea na waliokamatwa wanashikiliwa kwa mahojiano.
Katika hatua nyingine, Kamanda Kova alisema walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa wa makosa mbalimbali ya unyang’anyi kwa kutumia silaha Moshi Omari akiwa na pikipiki aina ya Honda Bajaj yenye namba T607 AQD ambayo ni ya wizi.
“Vilevile katika kuendeleza doria za kuimarisha ulinzi tumewakamata watuhumiwa wawili kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha ambao wameshiriki katika matukio mengi ya uhalifu hapa jijini,” alisema Kamanda Kova.
Aliwataja watu hao kuwa ni Jovin Deofin na Juma Athuman ambao wote ni wakazi wa Kongowe, Wilaya ya Temeke.

Ujerumani yampiga jeki mkaguzi mkuu wa Serikali

Kwa ufupi
Akizungumza jana wakati wa kusaini makubaliano ya msaada huo ambao umetolewa kupitia Shirika la Misaada la Ujerumani (GIZ), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, alisema msaada huo wa Euro 3.5 milioni utakwenda katika maeneo mbalimbali ya ukaguzi na kwamba mradi huo utakuwa wa miaka minne.
Dar es Salaam. Serikali ya Ujerumani imetoa msaada wa zaidi ya Sh7 bilioni kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za ukaguzi zinazofanywa na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT).
Akizungumza jana wakati wa kusaini makubaliano ya msaada huo ambao umetolewa kupitia Shirika la Misaada la Ujerumani (GIZ), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh, alisema msaada huo wa Euro 3.5 milioni utakwenda katika maeneo mbalimbali ya ukaguzi na kwamba mradi huo utakuwa wa miaka minne.
Alisema lengo la msaada huo ni kuboresha utendaji wa ofisi hiyo na kuhakikisha inatimiza wajibu wake kwa ufanisi katika ngazi ya kitaifa na kimataifa pamoja na kuboresha uhusiano na wadau wakuu wa nje. Alisema pia fedha hizo zitasaidia kuikagua Serikali na misaada wanayopewa na wafadhili ikiwamo Ujerumani.
“Msaada huu umekuja wakati muafaka hasa ikizingatiwa kuwa tangu Julai mwaka jana tumeanza shughuli za ukagu

ASANTE MAMA KWA KUTAMBUA HILO(JOYCE BANDA)


Today we celebrate the life of an African Child. While celebrating the life of an African Child, I believe we have a collective responsibility in eliminating harmful social and cultural practices affecting children in our communities.

I want to ensure everyone that my government will continue to prioritise the welfare of children in this country . We will continue to implement the Safe Motherhood initiatives as their outcomes have proved to be a success in promoting the safety of mothers and children. We will continue to implement the Economic Recovery Plans as the benefits are proving to reduce poverty at household level especially when prices of essential things like fuel have gone down.

I have also felt motivated to accelerate the implementation of the Mudzi Transformation Trust Initiative which is meant to bring the social and economic benefits per family because this is another way of combating poverty.

Let me also assure everyone that our government will continue to implement projects that will address issues of hunger and malnutrition and policies that will promote access to education for our children. We have a zero tolerance stance with regards to harmful practices on children ie child labour, child abuse and neglect because the welfare of children in this country is our number one priority.

As a matter of priority, we will listen to everyone on how best we can work together to make the lives of children better in this country because we are a listening government and because we are very passionate about children.

I take this opportunity to profoundly thank everyone committed to uplift the lives of children in this country. Your contribution is what brings joy to children, please continue with this selfless spirit of doing the best for children.

In my view, a child is like a garden, when one takes care of the garden it becomes glorified with beautiful flowers and landscapes making the entire community proud. Therefore I urge all of us to do our best, children are the future of this nation.

Have a blessed Sunday everyone .

And may God bless your children!

Dr Joyce Banda
President
Republic of Malawi

BINTI ACHOMWA MOTO HADI KUFA KWA KUOMBA AOLEWE NA MTU WA UKOO WAKE...

Anju Yadav (kushoto) na Ranjit Yadav.
Msichana wa miaka 19 amechomwa moto hadi kufa na mama yake kupigwa baada ya kuwaomba wazee wa kijiji kuruhusiwa kuolewa na mvulana mmoja kutoka kijijini hapo na ukoo mmoja, polisi wa India wamethibitisha.
Anju Yadav, kutoka kijiji cha Karahkol, wilayani Deoria katika jimbo la Uttar Pradesh, alichomwa moto nyumbani kwake wakati mama yake, Gyanwati Devi, mwenye miaka 48, alipokuwa upande mwingine wa kijiji hicho akiiomba halmashauri ya kijiji kumruhusu Anju aolewe na rafiki yake wa kiume aliyekuwa na mahusiano naye kwa miaka miwili, Ranjit Yadav, mwenye miaka 21.
Lakini halmashauri ya kijiji hicho, sambamba na baba wa mvulana huyo, Jai Hind Yadav, mwenye miaka 52, walitupilia mbali maombi hayo wakisisitiza ilikuwa kinyume cha utamaduni.
Badala yake, baba wa mvulana huyo alikimbilia kwenye nyumba ya familia na kumchoma moto msichana huyo, ilidaiwa.
Jamii ya India inafahamika mno kwa mfumo wake wa ukoo ulioingiliana, ambao unaweza kuzuia watu kutoka jamii tofauti kuoana na katika baadhi ya matukio kuafikiana na jambo kama hilo.
Hatahivyo, inaeleweka kwamba haikubaliki kwa watu kutoka ukoo mmoja na kijiji kuoana. Ndoa ndani ya Gotra (ukoo) mmoja pia hairuhusiwi katika utamaduni wa India, hasa katika mikoa ya kaskazini mwa nchi hiyo ambako makundi ya kiukoo, yanayofahamika kama Khap Panchayats, yanachukulia ndoa kama hizo kuwa kosa la jinai.
Rakesh Kumar, mkuu wa Kituo cha Polisi cha Ikauna, alisema: "Jai Hind pamoja na wanakijiji wengine watatu walikimbilia nyumbani kwa msichana huyo na kumwagia mafuta na kisha kuchoma moto wakati mama yake akiwa kwenye kikao hicho cha halmashauri. Tumewakamata wafuasi wawili wa kundi hilo wakati wengine wawili wakiwa wanaendelea kusakwa."
Anju aliungua asilimia 85 ya mwili wake wote na alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa hospitali Alhamisi jioni.
Anju alikuwa peke yake wakati wanaume hao wanne walipovamia nyumbani kwake. Katika kuchanganyikiwa aliruka kutoka kibarazani kwake hadi ghorofa ya pili kujaribu kujiokoa. Alivunjika mikono na miguu yake.
Wanakijiji walimmwagia maji, lakini wakati huo alikuwa tayari amepata majeraha makubwa ya moto.
Mama yake, Gyanwati, alisema wote binti yake na Ranjit walipendana sana na kudhamiria kufunga ndoa.
Gyanwati alikwenda nyumbani kwa Jai Hind Jumatano jioni kujadiliana kuhusu suala la ndoa lakini pale yeye na familia hiyo walipokataa alikwenda katika baraza la kijiji kwa msaada,  jambo la kawaida katika India.
Gyanwati alisema: "Nilitaka kumwona binti yangu akiwa mwenye furaha. Walipendana mno; sikuwa na tatizo na ndoa yao. Lakini pale nilipokwenda kwa Jai Hind na maombi hayo alinieleza ni dhambi kuoana ndani ya ukoo mmoja na hatokubaliana na ndoa hiyo."
Polisi wamethibitisha kwamba Jai Hind bado hajapatikana.

DR. MARY NAGU ANUSURIKA KUCHOMWA MOTO NA WAFUASI WA CHADEMA



WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu pamoja na Mbunge wa Babati Vijijini, Jitu Soni (CCM), wamenusurika kuchomwa moto na wafuasi wa Chadema usiku wa kuamkia jana.

Tukio hilo lilitokea usiku wa manane, baada ya wafuasi wa Chadema, wakiongozwa na Mbunge wa chama hicho Jimbo la Karatu, Mchungaji Israel Natse, kuvamia nyumba waliyokuwa wamefikia Nagu na Soni, katika Kata ya Bashnet, Babati Vijijini, mkoani Manyara.

Wafuasi hao wa Chadema wanawatuhumu Dk. Nagu na Soni kukutana katika nyumba hiyo kwa nia ya kupanga mipango ya kutoa rushwa ili kufanikisha uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata hiyo, unaotarajiwa kufanyika leo, ikiwa ni pamoja na maeneo mbalimbali nchini.

Chanzo cha MTANZANIA Jumapili kilichokuwa eneo la tukio kililidokeza gazeti hili kuwa Dk. Nagu na Soni

walikwenda kijijini hapo usiku, wakiwa na magari mawili, kila mmoja na lake na kufika nyumbani kwa mtu aliyetajwa kwa jina la Petro Baha, kwa kile kilichodaiwa kuwa ulikuwa ni mpango wa kupita na kugawa fedha kwa wananchi usiku huo, ambapo pia inadaiwa ndani ya nyumba hiyo alikuwepo mgombea udiwani wa Kata hiyo, Nicodemus Gwandu (CCM).

Kitendo cha Nagu pamoja na Soni kuonekana katika nyumba hiyo kiliwashitua wafuasi wa Chadema, ambao baada ya muda mfupi walivamia nyumba hiyo wakiwa na Mbunge wao, Natse, madiwani na msafara wa pikipiki na kutishia kuichoma moto.

Mtoa habari wetu huyo alisema kuwa, wafuasi hao wa Chadema waliweka kambi katika nyumba hiyo kuhakikisha Nagu na Soni hawatoki kwenda kwa wananchi usiku huo.

Chanzo chetu kilisema kitendo cha kuzingirwa huku wakitishia nyumba kuchomwa moto kiliwashitua viongozi hao wa CCM na kuamua kupiga simu polisi, ambao walifika wakiwa sita muda mfupi baadaye kwa ajili ya kuimarisha ulinzi hadi walipotoka jana asubuhi.

Inaelezwa kuwa mgombea wa udiwani wa CCM, Nicodemus, ambaye naye alikuwemo ndani ya nyumba hiyo pamoja na akina Nagu, yeye alifanikiwa kutoroka mapema kwa kuruka ukuta na kukimbia.

Alipotafutwa Dk Nagu ili kupata ukweli kuhusu taarifa hizo, simu yake ya kiganjani iliita bila mafanikio na hata alipotumiwa ujumbe mfupi nao hakujibu.

Kwa upande Soni, alikiri kuzingirwa na wafuasi hao wa Chadema, lakini alikanusha madai ya mkakati wa kutoa rushwa.

“Ni wanachama wa Chadema wakiongozwa na Mbunge wa Karatu, Mchungaji Natse na madiwani karibia wa kata sita pamoja na msururu wa pikipiki, sisi tulikuja kulala, mimi siku zote huwa nalala kijijini, sasa walikuja wakaanza kupiga yowe, ndipo wananchi wakatoka. Tulikuwa wanne na magari mawili,” alisema Soni.

Akielezea sababu za kwenda kulala katika nyumba hiyo, Soni alisema walifikia hatua hiyo baada ya kuwapo kwa mpango wa Chadema kufanya fujo.

Alisema dalili hizo zilianza kuonekana mapema baada ya Dk. Nagu kuwekewa mawe kwenye daraja la Kambesh, kitendo ambacho kilimfanya ashindwe kuondoka na kwenda kulala alipoandaliwa Soni.

Akifafanua tuhuma kuwa walikwenda kwa ajili ya kutoa rushwa, Soni alisema kama wafuasi hao wana uhakika wathibitishe madai yao.

“Waje wathibitishe rushwa gani ya kuwapatia watu wanne, maana ndio waliokuwemo katika nyumba hiyo, hata mgombea wanayedai alikuwepo alikuja hapo mara baada ya kusikia yowe, wananchi wamesaidia kuwatawanya,” alisema Soni.

Mbunge wa Chadema, Natse alikiri kuwepo katika eneo hilo, baada ya kupatiwa taarifa kwa njia ya simu na wananchi ambao walimweleza juu ya kuwako kwa mpango wa kutoa rushwa uliokuwa ukiandaliwa na Nagu pamoja na Soni.

“Kilichotokea saa 7 usiku tulipigiwa simu na wananchi kuwa Waziri Nagu na Soni walikuwa eneo la Bashnet, ambalo ndiyo ngome yao ya rushwa na walikwenda kugawa huko, lakini walipoonekana tu yowe lilipigwa na watu walikusanyika wakitoka na silaha, ikiwemo mapanga na mikuki,” alisema.

Natse alisema kuwa baada ya taarifa hizo walikwenda eneo la tukio ili kuepusha madhara zaidi, kutokana na wananchi hao kudhamiria kuchoma moto nyumba walimokuwamo vigogo hao wa CCM.

“Tulipofika tuliwatuliza wananchi, lakini waligoma kuondoka, lakini wao (kina Nagu) walikuwa wameshapiga simu polisi. Askari walipofika eneo la tukio tuliwataka wawatoe nje wahusika, lakini walitusihi tukubali wawalinde mpaka asubuhi asitoke mtu, suala ambalo wananchi waliliafiki, huku wao wenyewe wakiendelea kuwepo eneo la tukio kuhakikisha kuwa hawatoki kwenda kugawa rushwa mpaka majira ya saa 11 nilipoondoka hapo,” alisema Natse.

Uchaguzi huo unaofanyika leo katika kata ya Bashnet, unawashirikisha wagombea watatu ambao ni Nicodemus Gwandu wa CCM, Alois Gwandu wa NCCR Mageuzi na Laurent Tara wa CHADEMA, ambaye kabla ya kuhamia chama hicho alikuwa diwani wa kata hiyo kwa tiketi ya NCCR Mageuz

Kweli Lady JD anastahili kuitwa ANACONDA angalia pesa zote hizo alitunzwa juzi wakati Mwana FA mmmmmmh!!

Leo: Tanzania vs Ivory Coast

Fuatilia katika ukurasa huu matokeo ya mchezo wa fainali wa kutafuta tiketi ya Kombe la Dunia brazili kati ya Morocco na Tanzania, kundi C. Utakao fanyika uwanja wa taifa June 16, 2013. Kwa matokeo na ratiba bofya hapa.
Kupitia ukurasa huu utapata, msimamo, matokeo ya michezo ya kundi C dondoo kabla, baada na wakati wa mchezo huo, Tabiri matokeo pia katika ukurasa huu.
Pia moja kwa moja kupitia akaunti yetu ya twitter kwa hashtagg #PamojaTaifaStars unaweza pata zaidi. au Ukurasa wa Taifa Stars

Tiketi:  Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
Viti Bei ya tiketi Idadi ya watazamaji
Kijani 5,000 19,648
Rangi ya bluu 7,000 17,045
Rangi ya chungwa 10,000 11,897
VIP C 15,000 4,060
VIP B 20,000 4,160
VIP A 30,000 748

eam MP W D L GoalsGD Pts
0 Côte d'Ivoire 4 3 1 0 108 10
0 Tanzania 4 2 0 2 60 6
0 Morocco 5 2 2 1 81 8
0 Gambia 5 0 1 4 2-9 1

Morocco yashinda,kundi lazidi kuwa gumu.

Timu ya Taifa ya Morocco jana ilifanikiwa kuifunga timu ya Taifa ya Gambia kwa magoli 2-0 na kuipiku Tanzania katika msimamo wa Kundi C.
Mpambano ulikuwa mkali na Morocco walifanikiwa  kupata goli la kwanza katika dakika ya 3 kupitia kwa Barrada na kipindi cha pili Belhanda akaipatia goli la pili ikiwa ni dakika ya 51 ya mchezo,na kuiacha kabisa Gambia kuendelea kushika mkia kwa kuwa na pointi moja.
Kwa matokeo hayo Morocco sasa wanapanda hadi nafasi ya pili wakiwa na pointi 8 wakiachwa kwa pointi mbili na vinara wa kundi hilo Ivory Coast wenye pointi 10 ambao leo watakuwa wageni wa Timu ya Taifa ya Tanzania watakapopambana pale Jijini Dar es Salaam.
Pia matokeo hayo yanaifanya timu ya Taifa ya Tanzania maarufu kwa Taifa Stars kurudi hadi nafasi ya tatu ikiwa na pointi 6 ivo itahitaji kucheza kwa kujituma zaidi ili washinde katika mchezo wa leo na kujiweka katika nafasi nzuri yakuwania kufuzu kwa  kombe la Dunia mwakani 2014 litakalofanyika nchini Brazil.

Saturday, 15 June 2013

PHOTO: Huyu ndio Miss Iringa 2013


BREAKING NEWZZZZ......BOMU LALIPUKA KATIKA MKUTANO WA CHADEMA ARUSHA LEO HII

 
HABARI KUTOKA KATIKA JIJI LA ARUSHA LINASEMA BOMU LIMELIPUKA KATIKA MKUTANO WA CHADEMA  WA KUHITIMISHA MKUTANO WA   KAMPENI ZA UDIWANI  ULIKUWA  UNAENDELEA JIJINI ARUSHA
MLIPUKO HUO AMBAO HAUKUJULINA CHANZO CHAKE KWA HARAKA LIMELIPUKA KUTOKA KUSIKO JULIKANA NA KIONGOZI MMOJA WA CHADEMA ANASEMEKANA KUUMIA VIBAYA  KATIKA TUKIO HILO.
HABARI ZAIDI NA PICHA ZINAWAJIA

HUYU MISS TANZANIA VIPI TENA?

 
Haikuweza kufahamika mara moja za sababu za yeye kupiga picha hizo na jitihad za kumtafuta zinaendelea ili aweze kuzifungukia
Miss Dar Indian Ocean ambaye ni Miss Kinondoni namba 2 mwaka jana, Diana Hussein  hivi karibuni amejikuta akipata aibu baada ya picha yake ya utupu kuvuja,
Picha hiyo inayomuonesha Diana akiwa matiti nje, imesambaa kwenye mtandao wa simu wa BBM huku baadhi ya watu ‘wakifoadiana’. 
Baadhi ya marafiki wa mrembo huyo walisema kuwa wameshangaa kuiona picha hiyo kwani kwa wanavyomjua hawakutarajia.

Akiizungumzia picha hiyo, Diana alisema aliipiga kwa matumizi yake binafsi ila akashangaa kuona imesambaa mtandaoni.

IN MEMORY OF LANGA KILEO | WASIFU WA MAREHEMU (VIDEO ZA NYIMBO ZAKE NA BAADHI YA PICHA)



Juzi alhamisi jioni tulipata taarifa juu ya kifo cha msanii wa hip hop ex-member wa wakilisha. Ni mtaalamu na mwanamuziki stadi wa Hip Hop nchini aliyeweka wazi kuathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya.

 Ili kuonyesha anachukizwa, Langa alilieleza jarida moja la burudani kwamba anakusudia kuanzisha Taasisi ya kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya.

Alisema matumizi ya dawa hizo yaliathiri shughuli zake za muziki na hakuwa na jambo lolote endelevu katika muziki wake.

Kimuziki Langa alianzia kundi la Wakilisha akiwa na Witness Mwaijega na Sarah Kaisi, ambapo walikuwa washiriki wa mashindano ya muziki ya Cocacola Pop stars, yaliyofanyika nchini Afrika Kusini.

Wakiwa na kundi hilo walifanikiwa kufyatua kibao cha ‘Hoi’, ambacho kiliteka wapenzi wa muziki.

Baadaye Sarah Kaisi (Shaa) alijitoa. Lakini Langa na Witness walifyatua kibao cha ‘No Chorus’.


Baada ya hapo Langa alifyatua kibao chake cha kwanza akiwa mwanamuziki binafsi, ‘Matawi ya Juu’ ambacho Dj John Dilinga (JD) aliwahi kuelezea ni moja ya kazi nzuri kutoka kwake, licha ya dosari za matumizi ya lugha.

Hata hivyo Langa alionyesha yeye ni bora na ana kipaji cha muziki. Amekuwa shujaa kwa kuendesha kampeni kali za kupinga matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana. Serikali inapaswa kusaidia juhudi zake pamoja.

Huyu ni mmoja wa matunda ya shindano la muziki la Coca-Cola Pop Stars mwaka 2004 ambalo washindi wake waliounda kundi la Wakilisha.  Mbali ya Langa, wengine ni Sarah Kaisi `Shaa’ na Witness Mwaijaga `Witness’. Huo ndio uliokuwa mwanzo wa kung’ara kisanii kwa wakali hao, ingawa kwa sasa kundi hilo limesambaratika, kila mmoja akitamba kivyake.

Lakini kwa bahati mbaya, mmoja wao, Langa kwa miaka ya hivi karibuni hakusikika kabisa, jambo lililomlazimu mwandishi wa makala haya kumtafuta sababu za ukimya wake.


Haikuwa kazi rahisi, lakini hatimaye Langa alipatikana na bila kutafuna maneno alisema kwamba, alishindwa kufanya kazi baada ya kuwa `teja’ aliyekubuhu.

Yaani alizama katika matumizi ya dawa za kulevya kiasi cha kupoteza kabisa mwelekeo si wa kisanii pekee, bali hata kimaisha.

“Siyo siri, kilichokuwa kimenifikisha katika hali hiyo ni dawa za kulevya. Kwa miaka mitano nilitumia sana Cocaine, Heroin, bangi na pombe. Namshukuru Mungu sasa nimerejea katika hali yangu.

“Siamini kama nimenusurika kwa sababu madawa yalinitesa, nikafanya mengi ya ajabu yaliyoichukiza familia yangu na marafiki ikiwa pamoja na kuwa mwizi na mkabaji mitaani na nyakati za usiku,” anasema Langa ambaye kundi lao la Wakilisha lilitamba na nyimbo kama `Unaniacha Hoi’ na `Kiswanglish’.

Anaeleza kwamba, kwake hayo ndiyo aliyoyaona maisha yanayomfaa, akidai awali alikuwa amechoshwa kuishi kwa masharti kutoka kwa wazazi wake waliokuwa wanampa mwongozo wa maisha, lakini bila kujua akadhani `anachungwa’.

Kwamba, umaarufu na ngekewa ya kuzishika pesa katika umri mdogo kupitia muziki vilimtia kiburi zaidi, na hivyo kuamua kujitenga kabisa na familia yake iliyomlea kwa mapenzi mazito.

“Niliamini naweza kujitegemea kupitia kazi yangu ya muziki, nikajichanganya mtaani,” anasema kijana huyo aliyetoa kibao chake cha kwanza, Matawi ya Juu mara baada ya kusambaratika kwa kundi la Wakilisha kutokana na kila mmoja kuamua kujitegemea kimuziki. Na kweli, Matawi ya Juu ilidhihirisha kuwa Langa ni moto wa kuotea mbali katika fani. Aliweza kusimama kwa miguu yake na kutikisa.

Mwenyewe anasema: “Jina hilo la Matawi ya Juu lilidhihirisha hivyo pale video ya kibao hicho ilipotajwa kuwania Tuzo za MTV Base kwa upande wa hapa Bongo miaka michache iliyopita, kisha kutwaa Tuzo ya Kisima nchini Kenya.

“Moto huo uliwafanya baadhi ya wasanii wakongwe katika gemu ya Bongo Fleva kunitafuta na kunipa majukumu ya kushiriki katika kazi zao, ikiwemo Chagua Moja ya Farid Kubanda `Fid Q’.

“Baada ya kuona wakongwe wamekubali vitu vyangu na kuanza kunishirikisha…nikapata pia safari za nje ya nchi. Huko Nairobi (Kenya) niliweza kufanya kazi na vichwa vikali vinavyounda Kundi la Necessary Noise, Naaziz na Wyre (Kevin Wyre).

Anasema mafanikio hayo yalimtuma kufyatua albamu yake ya kwanza aliyoipa jina la Langa, akiamini itampaisha zaidi kimaisha na kimuziki. Hata hivyo, mambo yalikwenda kinyume. Anasema alipoipeleka sokoni, wauzaji wakubwa waliigomea, hivyo kumpa wakati mgumu wa kuwaza na hatimaye kujikuta akiongeza kasi ya matumizi ya dawa za kulevya.

Siyo siri, kugoma kwa albamu yangu sokoni kulichangia kasi ya kutumia dawa za kulevya…niliona ni njia pekee ya kuondoa mawazo kwa sababu kazi iligoma, na home (nyumbani) nilishaharibu.

Sikufanya tena kazi kwa umakini na kila kazi niliyoitia haikufanya vizuri….” Anasema kwamba, baada ya mambo kumwendea mrama, ndipo alipoanza kuiba vitu nyumbani kwao kwa lengo la kuviuza na inapotokea amekosa, alidiriki hata kupiga debe katika vituo vya mabasi ili mradi apate fedha za kununua `unga’.

Haikuishia hapo, kwani anasema alijiingiza katika kundi la wahuni waliojihusisha na wizi na ujambazi. “Kwa ujumla nilipoteza mwelekeo. Maisha yangu yakawa ya kutembea na kisu kama kitendea kazi changu katika wizi,” anasema huku akitikisa kichwa kama ishara ya kujutia matendo aliyoyafanya kwa msukumo wa madawa ya kulevya. Anakumbuka akiwa mtumwa wa `unga’, aliingia katika mikasa kadhaa ikiwa pamoja na kupigana na polisi baada ya kunaswa na dawa hizo haramu.

Katika wizi, chochote alichokikuta mbele yake kilikuwa halali. Anasema alikwapua vitu magengeni, madukani na hata magari yaliyoegesha vibaya alinyofoa vioo na mashine zinazosaidia kupandisha na kushusha vioo ndani ya gari.

“Ni matukio ya aibu. Yanasikitisha…,” anasema Langa anayedokeza kwamba, akiwa mtumiaji wa `unga’, alikuwa anakutana na wasanii na watu wengine mashuhuri. Hata hivyo anakataa kuwataja, akidai ni siri yake. `Ufufuo’ wa Langa kutoka katika lindi la mateso ya dawa za kulevya ulipatikana kuanzia Machi mwaka huu, baada ya familia yake kumpeleka kijana wao kwa tiba maalumu ya kuachana na matumizi ya `madudu’ hayo. Na kweli, elimu imemwingia na kujikuta akirejea ufahamu wake wa kawaida.

Ametangaza kuachana na `unga’, pombe, sigara na badala yake amejikita zaidi katika mazoezi ya kurudisha mwili wake katika hali ya kawaida. Aidha, amekata shauri la kuirudia fani yake na tayari ana vitu vipya, Bombokiata na Mteja Aliyepata Nafuu.

Anasisitiza kwamba, kutokana na mateso aliyoyapata, anakusudia katika siku za baadaye afungue kituo chake cha tiba ya dawa za kulevya ili aweze kuwaokoa vijana wengine wanaoangamia kutokana na matumizi ya dawa hizo haramu zinazopigwa vita karibu kote duniani. “Nimenusurika, namshukuru Mungu.

Nami najipanga kutaka kuwasaidia wengine waachane na mateso ya dawa za kulevya. Pia nichukue fursa hii kuwaomba msamaha wote niliowakosea kwa namna moja ama nyingine wakati nikiwa `teja’,” anasema Langa, kijana mwenye umri wa miaka 25.

Je, historia ya maisha ya Langa ikoje? Anasema Desemba mwaka 1985 jijini Dar es Salaam akiwa tunda la wanandoa Vanessa Kimei na mumewe Mengisen Kileo. Alisoma Shule ya Msingi Olympio na Sekondari ya Loyola, zote za jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, akiwa kidato cha pili alihamishiwa Kampala, Uganda katika Shule ya Vienna na baadaye Shule ya Hillside International Academy, huko huko Uganda. Baadaye alirejea nchini na kujiunga na masomo ya Stashahada ya Masoko katika Chuo cha Biashara Dar es Salaam (CBE), Kampasi ya Dodoma.

Huyo ndiye Langa Kileo msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye baada ya kulewa umaarufu na kujikita katika matumizi ya dawa za kulevya, ameibuka na kujutia `ujanja pori’, sasa akitaka kujiingiza katika kampeni ya kuwaokoa vijana wengine waliozama katika `unga’. Anakusudia pia kurudi darasani kujiendeleza na masomo ya elimu ya juu. Je, atafanikiwa? Kwa hakika, hili ni jambo la kusubiri na kuona.

Bomu lalipuka kwenye mkutano wa CHADEMA; watu kadhaa wahofiwa kupoteza maisha

Mungi ameripoti @ JamiiForums kuwa bomu limelipuka kwenye mkutano wa CHADEMA Arusha. Watu kadhaa wahofiwa kupoteza maisha, na wengine wajeruhiwa.

Kwa mujibu wa aliyetoa habari hii, inaonekana bomu hilo lilitegwa karibu na gari la matangazo. Mtoto aliyelipukiwa na bomu amefariki uwanjani.
arusha-bomu-chadema

BAADHI YA PICHA KUTOKA HOSPITALI ZA ARUSHA (TUKIO LA BOMU SOWETO,ARUSHA)

Baadhi ya picha ya moja ya video ya malaika toka kwa watoto wa nyumbani mafinga wakijipanga kuachia ngoma kali kuwa tayari kuipokea ngoma hiyo